Learn Swahili with SwahiliPod101!
Don't forget to stop by SwahiliPod101.com for more great Swahili Language Learning Resources!
-------Lesson Dialog-------
----Formal Swahili----
MCHANO WA NYWELE WA WANYAMA
AINA ZOTE ZA NYWELE
Watu wengeni huwa na michano ya nywele ya ajabu.
Nywele zao huwa na umbo ama rangi za ajabu.
Inaweza kuwa fupi, refu, laini ama kishenzi.
Wanyama wengi pia huwa na michano ya nywele za ajabu.
Aina zingine za michano ya nywele zinaweza kukushangaza ama kukufanya ucheke.
MBWA
Je, shungi zako huanguka ndani ya macho?
Mbwa aina ya kondoo wa enzi za kale nchini Uingereza wanashinda hiyo.
Aina hii ya mbwa inajulikana kwa nywele ndefu na isiyochanika.
Nywele yake inapaswa ichanuliwe mara kadhaa kwa wiki.
Komondos ni aina nyingine ya mbwa aina ya kondoo.
Wako na nywele inayokaa kama kamba.
Kamba zinazoweza kukua na urefu wa hadi futi moja.
Komondos wako na nywele nyingi kuliko mbwa mwengine wowote.
Baada ya kuoga, nywele zao huchukua siku mzima kukauka.
Mbwa wa Afghan huvaa nywele ambao umenyooka.
Kama kondoo aina ya mbwa, nywele zao huhitanji kutunzwa vizuri.
Aina hii ya mbwa mrefu lazima ioshwe na kupambwa mara mbili kwa wiki ili huhifadhi nywele zao vizuri.
PAKA
Paka wa kiajemi hujulikana kwa nywele mrefu.
Hakuna anayejuwa jinsi paka wa kwanza wa nyumbani alipata nywele mrefu.
Paka wa nyumbani walitoka kwa paka mwitu wa Afrika, wako na nywele fupi.
Paka nyumbani wa kwanza walijulikana miaka elfu kumi iliyopita.
Paka wa Kiajemi wa kwanza alijulikana kutoka 1871.
Himalayans ni mchanganyiko wa Kiajemi na paka wa Siamese.
Wako na nywele refu ya Kiajemi na mipororo za Siamese.
Mwili mweupe na miguu nyeusi, uso, masikio na mkia zinaitwa rangi ya pointi.
SUNGURA NA NUNGUBANDIA
Je, unaweza jua jinsi sungura kichwa-simba walivyopata jina zao?
Kama simba wa kiume, wako na nywele mrefu inayoitwa shugi kwenye kichwa.
Wakulima walichanganya aina mbili ya sungura, wakidhani watapata sungura mdogo aliye na nywele.
Mshangao! watoto walikuwa na nywele mrefu, lakini kwa sehemu fulani pekee.
Aina kadhaa ya nungubandia wako na kapa mrefu.
Texeli wako na manyoya nyororo ambayo imefunika mwili yote.
Coroneti wengine wako na sehemu kwa nywele zao.
Wengine nywele imemea kama umbo la maua vichwani mwao.
WANYAMA WALIO NA KWATO
Ngombe wa mlima hufugwa Uskotini.
Wako na nywele refu la kiwimbi ambayo huwaweka joto wakati wa manjira ya baridi.
Kwa sababu ya nywele zao nzito, hawa wanyama hawawezani na hali ya hewa ambayo ni ya joto.
Fahali wa meski pia wako kwa familia ya ngombe.
Wako na nywele nzito ya kuwapasha joto katika msimu mrefu wa baridi nchini Grinlandi na Kanada.
Nywele zao huwafanya waonekane wakubwa kuliko walivyo.
Rackas ni aina ya kondoo kutoka nchi ya Hungaria.
Wako na manyoya refu ambazo huwa nyeupe ama nyeusi.
Wote wa kiume na wa kike huwa na pembe mrefu zilizojizungusha.
Wa kiume waweza kuwa na pembe zaidi ya urefu wa fiti mbili.
Nguruwe walio na ndevu huishi msituni kusini-mashariki mwa Asia.
Walipewa jina hili kutokana na ndevu zao ambazo humea kwa kinywa.
Nguruwe wengine huwa na ndevu ama nywele ndefu ya shavu.
Wengine wako na masharubu na nywele nyingi.
Nywele zingine kwa upande mwingine wa mwili huwa fupi.
NYANI NA KOMBA
Nyani wa colobusi wako na unyoya mweusi ambao hufunika mwili mwote.
Kofia mrefu imeenda upande upande mpaka kwa mgongo.
Pia wako na ndevu nyeupe na nywele nyeupe kwa mkia.
Simba wa thahabu ni nyani ambao huishi katika msitu mmoja tu ulioko Brazil.
Nywele zao ni nyekundu na kungaa-rangi ya machungwa, kama moto.
Nyani hawa wako na sura ambayo haina nywele lakini imezungukwa na shungi.
Empaya taramani ambao ni binamu, wako na masharubu mrefu nyeupe.
Geladas ni nyani wakubwa ambao ni binamu wa sokwe.
Mwili wao umefunikwa na nywele ngu [...]