Sepetuko

Kupunguzwa kwa Washauri Serikalini


Listen Later

Mkuu wa Utumishi wa Umma Felix Koskei amewaandikia Mawaziri wote kuwataka kupunguza idadi ya washauri kutoka wawili hadi mmoja kwa kila Waziri ili kupunguza matumizi ya pesa za serikali. Hatua hii imeibua swali la hivi hawa washauri wamekuwa wakifanya kazi gani ikiwa kwa kipindi cha miaka miwili serikali hii imekuwa ikifanya baadhi ya maamuzi mabovu mno, kiasi cha kugeuka na kuwa shubiri kiasi hiki? Je, washauri hawa wamefeli katika majukumu yao au ushauri wao umekuwa ukipuuzwa na viongozi wanaoshauriwa?
...more
View all episodesView all episodes
Download on the App Store

SepetukoBy Standard Media