Mara nyingi mwanamke anapovishwa pete ya uchumba, hutarajia kwamba aliyemvisha pete hiyo atamwoa. Hata hivyo, kijana mmoja amejipata kwenye njia-panda kwani hata baada ya kumvisha mpenziwe pete ya uchumba, hana hakika kama atamwoa au la kwani kijana huyo anasisitiza kwamba ni lazima waishi kwenye eneo moja na mchumba wake atakapomwoa ilhali mchumba huyo anaishi katika kaunti nyingine anakofanyia kazi. Je, msichana huyo aache kazi ili aishi na mpenziwe? Tunalidadavua suala hili.