PWANIFM PODCAST

NYUWI SI UTSAI


Listen Later

Makala haya ya Nyuwi si utsai ni makala kwa lugha ya kigiriama

 kutoka  jamii ya mijikenda yanayozungumzia kuhusu
kukomesha visa vya mauaji ya wazee kwa kisingizio cha uchawai.

Kwa zaidi ya miaka kama miaka mitatu iliyopita wazee wengi

katika kaunti ya Kilifi wamekua wakiuliwa kwa kusingiziwa kuwa ni wachawi hali
ambayo imeleta wasiwasi mkubwa kwa jamii ya kaunti hio.

Kila mwaka wazee 150 huuliwa hii nikulingana na shirika la utunzi

wa mila na damaduni za mijikenda MADCA .

Ndio sababu iliyonifanya kuzama na kuja na makala haya

ambapo niliongea na spika wabunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire ambaye
anasema kuwacha mila na kukumbatia mila za kigeni ndio chanzo cha watu kuwaona
wazee kama tishio kwa maisha yao.

Pia ukosefu wa ajira nao umetajwa kuchangia kwa vijana

kutamani utajiri wa haraka bila jasho hali ambayo huwafanya kuwaua wazee wao
ili warithi mali.

Mzee Stanlus Kiraga wa MADCA anasema kuwa zamani ucgawi

ulikua ukitumika kulinda mamboma ya jamii ya mijikenda lakini siku hizi watu
wamekosa kuuelewa na wameanza kuwaroga wenzao.

Chidongo naye anasema vijana wakiota ndoto mbaya tu basi

huanza kuwashuku wazee wao hali inayochochea mauaji hayo.

Mwambire anasema watu wakija pamoja na kuelewa mila na

desturi za mijikenda hali hii itakomeshwa.

...more
View all episodesView all episodes
Download on the App Store

PWANIFM PODCASTBy PWANIFM PODCASTS