Podcast hii inamwangazia jamaa mwenye umri wa miaka 30 ambaye hajui la kufanya baada ya mkewe kumtoroka. Kijana huyo anayefanya kazi katika Kaunti ya Isiolo anasema kwamba siku moja mkewe alimwomba ruhusa ya kwenda kuwaona wazazi wake na hadi sasa hajarejea. Mwanamke huyo aliondoka pamoja na mtoto wao wa umri wa miaka 3 na anapopigiwa simu na mumewe anasema kwamba aliolewa kwingine. Kijana huyu yuko katika njia-panda asijue la kufanya. Mshauri wa masuala ya kijamii, Rachel Mahungu anampa ushauri katika podcast hii.