Mitandao ya kijamii ikiwamo Facebook, WhatsApp, Twitter, Instagram na kadhalika imerahisisha pakubwa njia za mawasiliano katika karne hii. Ni hali ambayo imechangia kubadilika kwa mbinu za watu kuchumbiana ambapo wengine hutumia mitandao kuwatafuta wachumba. Lakini je, hili linafaa? Tumehusisha kauli za wananchi kuhusu mapenzi ya mitandaoni vilevile kushiriki mazungumzo na vijana na washauri wa masuala ya kijamii kuihusu mada hii.