Wasichana wa Kenya wanaeleza sababu za kuwapenda wanaume wa Nigeria au Wazungu; kwamba wanajua mapenzi, kutumia pesa, kuvinjari na kuwapa raha za peponi. Kwamba wanaume wa Kenya hawajui kupenda, wana mikono birika. Ni gumegume tu...si wanaume kamili. Nao wanaume wa Kenya wanahofia ushindani na kusalimu amri; wanasema kwamba ni sawa tu...acha wapendane.