Ukatili wa kijinsia, ni unyanyasaji ambao huelekezwa kwa mtu mmoja kulingana na jinsia yake ya kibaolojia AU utambulisho wa jinsia. Inajumuisha unyanyasaji wa mwili, kijinsia, matusi, kihemko, kisaikolojia, vitisho, kulazimishwa, na kunyimwa uchumi au elimu, dhuluma hii, iwe hutokea katika maisha ya umma au ya kibinafsi. Watu wengi kwa kuogopa kubaguliwa, wanaepuka kuripoti hili jinamizi. Jiunge nami katika mazungumzo ya leo na Bramwel Wabwire almarufu kama Kaka Bramsey, Bramwel alikuwa mkurugenzi wa zamani wa masomo wa baraza la wanafunzi wa chuo kikuu cha karatina. Alipata kesi kadhaa za udhalilishaji wa kijinsia zilizowekwa kwenye dawati lake, katika majadiliano, anafunua jinsi ilivyoshughulikiwa na changamoto kadhaa ambazo wahanga wanakabiliwa nazo, mimi ndiye mwenyeji wako simiyu nalianya na hii ni arctivate podcast tuingie kwenye mjadala sasa. Karibu