Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu? AYUBU 9: 2
Kuna swali la dharura na la muhimu linalomkabili mwanadamu, swali lililoulizwa zamani na Ayubu: "Mtu huwaje kuwa mwenye haki mbele za Mungu?"
Kadri tunavyo endelea, vivyo hivyo shida duniani zinaongezeka. Utalamu wa kuzishugulikia pia unaongezeka na kadhalika. Mabadiliko ni mengi.
Mungu wa milele, "Baba wa mianga, kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka ”(Yakobo 1:17).
Shida kuu kwa mwanadamu sio yeye mwenyewe, furaha yake, au hali zinazomzunguka wakati yuko hapa duniani. Shida yake kuu ni uhusiano wake na Mungu; na Mungu ni wa milele, habadiliki, ni mkamilifu.
Ni kweli kusema kwamba katika nyanja nyingi na idara za maisha ya hivi karibuni bila shaka ni Bora. Kwa mfano, kupungua kwa kiwango cha vifo kwa magonjwa kama uti wa mgongo na nimonia kweli ni ya kushangaza. Hatuwezi kuwa na swali kabisa katika matibabu ya magonjwa ya mwili, ya hivi karibuni kua ni bora. Na hata maendeleo ya fani mbali mbali.
Lakini je! Hiyo inaweza kusemwa juu ya tiba ya magonjwa ya roho? Je! Mbinu ya kisasa ya kutibu dhambi ipo?
Ni upumbavu kwa mtu wa kisasa kutafuta suluhu kwenye Uvumbuzi au wokovu aina nyingine badala ya "Habari Njema ya utukufu wa Mungu ”(1 Timotheo 1:11), ambayo inapatikana peke yake katika Bwana wetu na Mwokozi, Yesu Kristo