Learn Swahili with SwahiliPod101!
Don't forget to stop by SwahiliPod101.com for more great Swahili Language Learning Resources!
-------Lesson Dialog-------
----Formal ----
Kuja kuzaliwa
Hiki kitabu cha kuvutia kimeandikwa na Marjorie Oludhe Macgoye mzaliwa wa uingereza ambaye amekuwa mkazi wa nchi ya Kenya kwa muda mrefu.
Wahusika wakuu katika hii hadithi ni Martin na mkewe Paulina ambao wamefunga ndoa hivi karibuni.
Katika mwanzo wa hadithi, Paulina ambaye ana umri wa miaka 16 ni mjamzito.
Anasafiri kutoka kijijini hadi mji mkuu wa Nairobi kujiunga na mumewe anayeishi na kufanya kazi Kariokor.
Inatokea kwamba baada ya siku chache, Paulina anakuwa mgonjwa na kupelekwa katika hospitali ya pumwani.
Kwa bahati mbaya ile mimba inatoka.
Analazwa hospitalini lakini siku ya pili anaamua kutoka na kuelekea nyumbani bila kumngojea mumewe.
Kwa bahati mbaya anapotea njia na kwasababu hafanikiwi kufika nyumbani, inamlazimu aishi nje kwa siku mbili.
Hatimaye, Martin anampata lakini amekasirika kwavile Paulina hakumngojea.
Usiku huo na kwa mara ya kwanza anamchapa bibiye.
Hadithi hii inaendelea na Paulina anapata mimba zingine lakini zote zinatoka kabla ya wakati wa kujifungua.
Ndoa yao inazidi kuwa ngumu, na kutofautiana pia kunaongezeka.
Martin anaanza kutokuwa mwaminifu na kuanza uhusiano na wanawake wengine.
Paulina naye anaamua kumuacha na kuelekea Kisumu.
Huko anafanikiwa kupata kazi ya uwalimu.
Naye pia anabadilisha mienendo na kuanza kuhusishana na mwanaume mwingine.
Chakushangaza ni kuwa wakati huu anafanikiwa kujifungua mtoto wa kiume.
Furaha yake inakatizwa wakati mtoto huyu anauliwa na polisi wanapofyatulia umati risasi katika mji wa Kisumu.
Paulina anaamua kurudi Nairobi ambapo anaajiriwa kama mjakazi kwa tajiri mmoja ambaye yuko katika harakati za siasa.
Martin anaanza kumtembelea Paulina na wakati kitabu hiki kinamalizika wameshakuwa mume na mke tena.
Mara hii, Paulina anafanikiwa kumpa Martin mtoto.
----Formal English----
Coming to Birth
This is a very interesting book written by Marjorie Oludhe Macgoye, a British-born lady but who has been a resident of this country for quite a long time. The story revolves around two main characters, Martin and Paulina who have just been married. At the beginning of the story, Paulina, who is 16 years old and pregnant, is traveling from the countryside to join her husband Martin who has just secured a job in Nairobi city at a place called Kariorkor. It happens that after some days, Paulina falls sick and is taken to Pumwani maternity hospital but unfortunately, she has a miscarriage. She is admitted to the hospital but before her husband comes to take her home, she finds her way out and she is unable to locate their home. She stays out for two days and finally Martin is able to find her and at this time he is very upset because she did not wait for him and has caused him a lot of trouble and that night he beats her up for the first time. The story continues as Paulina continuously miscarries and the marriage is becoming tough for both of them. Martin has now started going out with other women and Paulina decides to leave for Kisumu where she is employed as a teacher. At this time, she also becomes unfaithful and gets pregnant with another man but this time round she is able to carry the pregnancy to the end and gives birth to a boy child. The boy is later shot dead by soldiers firing at a crowd in Kisumu. She goes back to Nairobi and is employed as a housekeeper by one rich family who are busy campaigning. Martin starts passing by Paulina’s house and as the book is ending, they are back together and she is able to give him a child.
---------------------------
Learn Swahili with SwahiliPod101!
Don't forget to stop by SwahiliPod101.com for more great Swahili Language [...]