SIRI ZA BIBLIA

MATHAYO 22: YESU AFAFANUA KUHUSU KIAMA


Listen Later

30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni.

31 Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema,
32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.
33 Na makutano waliposikia, walishangaa kwa mafunzo yake.
34 Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja.
35 Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu;
36 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
37 Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.
41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo?
42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.
43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,
44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?
45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?
46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena.

...more
View all episodesView all episodes
Download on the App Store

SIRI ZA BIBLIABy SIRI ZA BIBLIA


More shows like SIRI ZA BIBLIA

View all
TIMIZA MALENGO YAKO by Joel Arthur Nanauka

TIMIZA MALENGO YAKO

5 Listeners

Timiza Malengo by Joel Nanauka

Timiza Malengo

0 Listeners

Innocent Morris by Innocent Morris

Innocent Morris

0 Listeners