Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

16 MEI 2024

05.16.2024 - By United NationsPlay

Download our free app to listen on your phone

Download on the App StoreGet it on Google Play

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Bahrain kwenye mji mkuu Manama, ambako wajasiriamali wamekusanyika kwa lengo la kutumia ugunduzi na ujasirimali kusongesha SDGs. Pia tunakuletea muhtasariwa habari kutoka ICJ, WHO na huko huko Bahrain, pamoja na uchambuzi wa neno “HIZAYA.”Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amerejea wito wake wa kutaka usitishwaji wa mashambulizi huko Rafah kwani wananchi wanazidi kuteseka kutokana na kulazimika kuhama kila wakati huku wakikosa huduma muhimu za kijamii ikiwemo msaada wa chakula na matibabu. Hii leo Mahakama ya Haki ICJ inasikiliza ombi kutoka taifa la Afrika Kusini ambalo linaiomba mahakama hiyo kuliwekea vikwazo zaidi jeshi la Israel ambalo linafanya mashambulizi ya anga na ardhini huko Ukanda wa Gaza mashambulizi ambayo yamegharibu maelfu ya maisha ya watu.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO hii leo limetoa muhtasari wa ugonjwa wa kipindupindu ulimwenguni ambao mpaka sasa umetajwa kuenea katika mataifa 24 katika kanda tano za shirika hilo huku Afrika ikirekodi idadi kubwa ya wagonjwa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “HIZAYA.”Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

More episodes from Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu