NINI KITATOKEA KABLA YA KUYAFIKIA MAFANIKIO YAKO? ๐๏ธ
Kabla hujafika kwenye maisha unayoyaota, kuna kipindi ambacho utajiuliza kama kweli uko kwenye njia sahihi.
Utakutana na rejection. Utapoteza pesa. Utapoteza watu. Utaona wengine wanakupita. Utafanya kazi bila kuona matokeo. Na kuna muda utaanza kujiuliza kama kweli unaweza.
Tatizo ni kwamba, wengi huchukulia temporary defeat kama permanent failure.
Wanashindwa mara chache, wanaona wamefeli. Wanajaribu biashara, haifanyi vizuri, wanaacha. Wanaanza kujenga kitu, hawapati attention, wanakata tamaa. Wanapitia kipindi kigumu, wanaamini maisha yamewaambia โhii sio njia yako.โ
Lakini vipi kama hicho kipindi hakijaja kukuambia uache?
Vipi kama kimekuja kukufundisha, kukujenga na kukuandaa kwa kile unachokisaka?
Katika episode hii tunazungumzia mambo ambayo yanaweza kutokea kabla hujafikia mafanikio yako, kwa nini kushindwa hakumaanishi safari imeisha, na kwa nini unatakiwa kujifunza kuanza tena unapopigwa na maisha.
๐ง NINI KITATOKEA KABLA YA KUYAFIKIA MAFANIKIO YAKO!
Sikiliza episode hii mpaka mwisho.
Na ukumbuke:
Temporary defeat si mwisho wa safari.
โ MWANAHISABATI Arthur Geil