Zaidi Shilingi Trilioni 5 ya Tenda za serikali iliyotengwa kwa ajili ya makundi maalum yaani vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu inakusubiri wewe?
Sikiliza msimu mpya wa Tenda Radio. Jumatano hii tukupe code ya kupata sehemu ya fedha hizo kwa kufanya kazi na serikali kupitia ununuzi wa umma kwenye mfumo wa NeST kwa watu wenye ulemavu.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uthibiti wa Ununuzi wa Umma Bw.Denis Simba atafunguka kuhusu jinsi ambavyo fursa za Tenda zimeongezeka kwa ajili ya Makundi Maalum kwa mwaka wa fedha 2025/2026
Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Kikwete,Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) atasikika.
Wabunge wanaowakilisha watu wenye ulemavu Bungeni nao watazungumza bila kusahau watu wenye ulemavu waliopata Tenda za Serikali nao watueleza wao wamewezaje.