Living Theology

YESU UFUNUO WA BABA


Listen Later

Aliyeniona mimi amemwona Baba. (YOHANA 14: 9)
Kristo alikuja ulimwenguni ili tupate kumjua Mungu kama baba yetu. Swali ni kuwa Yeye humfunuaje Baba kwetu?
Hapo katika Injili utapata ya kwamba Kristo alimfunua katika maisha yake mwenyewe kwa kuishi maisha yasiyo na doa na yasiyo na dhambi. Alipohukumiwa, Aligeuka kwa wale waliomshtaki na kusema, "Je! kuna mtu yeyote aweza kuninyooshea kidole? Je! waweza kunihukumu juu ya kushindwa kwokwote kwa maswala ya Mungu au sheria? ” Maisha yake yalikuwa ya kipekee; yalikuwa makamilifu; na kwa hiyo basi Alimfunua Mungu kwa kuwa jinsi Yeye alikuwa.
Pia akamfunua Mungu kwa matendo yake:- katika miujiza Yake. Tunaona  Aliwainua watu kutoka kwa wafu, kuponya wagonjwa, kusababisha kuona kwa vipofu na kadhalika.
Mambo haya katika Agano Jipya ni  muhimu yanayotuonyesha Mungu katika mwili. Sio vigumu kutarajia miujiza ikiwa Mungu katika mwili yuko hapa, na ndivyo Kristo anavyodai kuwa. Mwangalie katika mambo ambayo Yeye hutenda.
Kisha, anamfunua Baba katika mafundisho yake. Aliiweka hivi: "Aliyeniona mimi amemwona Baba" (Yohana 14: 9). Kabla tu ya Mwisho wake, Filipo akamwambia, "Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha ”(Yohana 14: 8) . Filipo akasema, " tuonyeshe Baba nasi tutaridhika” Kwa asili, Bwana wetu akajibu, "Nitazame, Filipo - angalia maisha yangu na matendo yangu. Nitazame, na ikiwa utafanya hivyo na kuniona kweli,basi umemwona Baba. ”
...more
View all episodesView all episodes
Download on the App Store

Living TheologyBy Brendon Naicker

  • 3
  • 3
  • 3
  • 3
  • 3

3

1 ratings