Learn Swahili with SwahiliPod101!
Don't forget to stop by SwahiliPod101.com for more great Swahili Language Learning Resources!
-------Lesson Dialog-------
----Formal ----
Jaguar
Charles Njagua Kanyi ni mwanamuziki wa Kenya anayejulikana kwa wengi kama Jaguar.
Yeye ni stadi kwa kufoka kiasi ya kwamba hawezi kosa kutambulika anapoigiza.
Alianza kazi ya muziki hapo awali na wimbo wa kwanza alioimba pekee ni 'Utaweza Kweli?'.
Nyimbo nyingine zake ni kama vile 'Kigeugeu', 'Fanya Mambo', 'Nikusikize', 'Nimetoka Mbali', 'Nimevuma', 'Tayari' na 'Unawasha'.
Aliutoa wimbo 'Kigeugeu' mwaka wa 2011 na bado anafurahia mafanikio yake hadi leo.
'Kigeugeu' ni video yake inayotazamwa sana hapa Kenya.
Hata hivyo, Jaguar ana utata mwingi unaomzingira, na anaugumu wa kujitoa katika utata huo.
Ili kukabiliana nao, aliitoa video ya kazi ya fadhila katika kaunti ya Turkana.
Katika video hii, alionekana akichangia wakaazi wa kaunti ya Turkana chakula.
Jaguar amefanya maonyesho yake Nairobi na Minnesota.
Pia, ameshinda tuzo kadhaa ikiwamo msanii bora wa kiume wa mwaka 2011 katika Shanga la Tuzo la Muziki la Afrika, msanii bora wa muziki aina ya boomba wa mwaka wa 2011 katika tuzo la Kisima; tena, alikuwa mmoja wapo wa wasanii bora wa kiume mwaka wa 2011 katika kitengo cha rika.
Hata hivyo,video ya 'Kigeugeu' ndiyo imeshinda tuzo nyingi.
Mbali ya kuwa mwanamuziki, Jaguar ni mwanabiashara, na alitajwa miongoni mwa wanamuziki tajiri sana nchini Kenya.
Yeye anamiliki msafara wa magari yanayojulikana kama 'Jagz cabs' na pia anamiliki karakana katika eneo ya viwanda, jijini Nairobi.
Pia, anamiliki nyumba yenye thamana ya milioni kumi na tano na magari manne yenye thamana ya milioni ishirini.
Yeye hupata angalau shillingi elfu mia tatu katika monyesho yake ya muziki.
Aidha, Jaguar anamiliki magari kadhaa ya usafiri kwa umma yanayotumika katika njia kadhaa mjini Nairobi.
Isitoshe, anamiliki kampuni ya usalama.
----Formal English----
Jaguar
Charles Njagua Kanyi is a Kenyan musician who performs under the name Jaguar. He is a very outstanding rapper who can hardly go unnoticed onstage. He started his music career long ago, and his first single was "Will U Really Make?" He has also done other songs, such as "Camouflager," "Do Things," "I Listen to You," "I Have Come from Far," "I Have Spread," "Ready," and "You Irritate." He released "Camouflager" in the year 2011 and still enjoys its success up to today. "Camouflager" is his most-viewed video in Kenya. However, Jaguar has a lot of controversy surrounding him, and it's proving hard for him to get rid of it. To counter it, he released a video of him doing charity work in Turkana County. This video features him donating food to the Turkana people.
Jaguar has performed in Nairobi and Minnesota and has also won several awards, including the Best Male Artist in 2011 at the Pearl of Africa Music Awards and the Best Boomba Artist in 2011 at the Kisima Awards, and he was one of the Best Male Artists in 2011 in the Urban Contemporary category. However, the video "Camouflager" has won the most awards.
Apart from being a musician, Jaguar is a business man and is cited among the richest musicians in Kenya. He owns a fleet of cars popularly known as "Jagz cabs" and a garage in an industrial area of Nairobi. He also owns a home worth 15 million and four cars worth 20 million. He gets at least 300,000 shillings for an appearance in his musical career. In addition, Jaguar owns several public transport vehicles that ply several routes in Nairobi. He also owns a security company.
---------------------------
Learn Swahili with SwahiliPod101!
Don't forget to stop by SwahiliPod101.com for more great Swahili Language Learning Resources!