Rafiki, tunaendelea na uchambuzi wa kitabu cha Wagalatia sura ya 6 katika sura hii Mtume Paulo anawashauri waamini kuhusu umuhimu wa kusaidiana na kubeba mizigo ya wengine. Anasema kuwa, kama mtu anapotenda dhambi, wale walio simama imara wanapaswa kumsaidia kurejea katika njia sahihi kwa upole na upendo.
Aidha, anawatia moyo waamini kutokukata tamaa katika kutenda mema, kwa sababu muda wa kuvuna utakuja. Zaidi ya hayo Mtume Paulo anasisitiza umuhimu wa Wakristo kuenenda katika roho.