Katika filamu hii ya “My name”, yaani jina langu, tunakutana na binti mrembo Yoo Ji Woo, ambaye katika maisha yake amekuwa akilelelewa na baba yake tu.
Kwa jinsi baba yake alivyokuwa akimpenda sana, basi Jiwoo anaweza kujiita “dad’s daughter” kama vile wadada huwa wanajigamba.
Maisha ya Jiwoo na baba yake siyo mazuri sana, kwani baba yake hakuwa na kazi rasmi ya kuwaingizia kipato zaidi ya kuwa mtu tuanayejihusisha na kazi haramu au tunaweza kumuita ‘gangstar’
Licha ya umaskini wao, maisha ya upendo na furaha yalikuwa ni kila kitu.
Maisha ya Jiwoo yanakuja kubadilika siku ambayo anatimiza miaka 17, kwani siku hiyo baba yake anaaga dunia kwa kupigwa risasi tena mbele ya macho yake.
itakuaje? Ji Woo atalipiza kisasi na kumsaka muuaji wa baba yake? Fuatili simulizi hii mpaka mwisho.