TANAPA Podcast Episode 05 inaangazia mwendelezo wa mada inayoeleza elimu ya Uhifadhi iliyohusisha Mila, Tamaduni, Desturi na Miiko anuwai iliyozuia baadhi ya wanyamapori kuuwawa lengo likiwa ni kuhifadhi maliasili zilizokuwa ndani ya maeneo yaliyohifadhiwa ambayo baadhi yake kwa sasa ndio Hifadhi za Taifa tunazozishuhudia zikitiririsha nyomi ya watalii nchini.
Eneo: Hifadhi ya Taifa Serengeti
Mwongozaji: Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Catherine Mbena
Wageni: Barnabas Murigo, Kenyatta, Musoka na Stanslaus Mayani
Usikose kila Jumatatu saa 11:00 jioni kupitia TANAPA Podcast.
TANAPA PODCAST, HIFADHI ZETU, SAUTI YETU.