Learn Swahili with SwahiliPod101!
Don't forget to stop by SwahiliPod101.com for more great Swahili Language Learning Resources!
-------Lesson Dialog-------
----Formal ----
MAISHA YANGU GEREZANI
Kitabu hiki kimeandikwa na John Kiriamiti aliyezaliwa tarehe 14 Februari mwaka wa 1950 Murang'a, nchi Kenya.
Alikamatwa na kupelekwa gerezani kwa miaka ishirini ambapo aliweza kuandika riwaya zake zinazo tambulika.
Riwaya hii inaanza na Jack Zollo anapowasili katika Mahakama ya sheria ya Nairobi ambapo alihukumiwa kifungu cha miaka ishirini gerezani na mijeledi arobaini na nne.
Jack anaudhika zaidi kwa muhula aliopewa huko jelani kiasi kuwa anazua vurugu nakuanza vita na askari wa jela na pia na wafungwa wenzake.
Anajifanya kana kwamba yeye ni mwenda wazimu ambapo analazwa katika taasisi ya akili kwa sababu ya ile hali yake ya wazimu na baadaye anatoroka kutoka kwa hospitali ya akili ya Mathare.
Hata hivyo, uhuru wake unadumu masaa kidogo tu ambapo anakamatwa tena na kurudishwa gerezani.
Jambo hili halimvunji moyo Jack Zollo ilhali anajitia moyo kuishi maisha magumu jelani anapokula kiazi kimoja kwa siku.
Jelani, Zollo anasimulia vituko vyake na vile mara kwa mara alivyokuwa kwenye vita na mawakala wa nchi na vile alivyoshinda jiji.
Ingawa mjini inambidi atoroke mara kwa mara maajenti wa sheria na wa amani ili aweze kuepuka kurushwa gerezani,
Zollo anaonekana mwenye kusherehekea maisha mazuri jelani na kuamua kuendelea kuishi pale gerezani licha ya ugumu.
Ana kuwa mashuhuri jelani kwa wafungwa wenzake na askari wa jela.
Kuongezea, anakuza ujasiri wake katika maishani yake ya jela.
Anatoka gerezani kama mtu aliyefanikiwa jelani na jijini huku akihusisha umaarufu wake kwa kuwa jambazi kabambe.
Jela linakuwa jiji kwa Zollo.
Kwake hakuna mpaka kati ya jela na jiji.
----Formal English----
My Life in Prison
This book is written by John Kiriamiti, who was born on February 14, 1950 in Murang'a, Kenya. He was arrested and imprisoned for twenty years, where he wrote some of his popular novels. The novel begins with Jack Zollo arriving at the Nairobi law courts where he is charged and sentenced to twenty years in prison and forty-eight cane strokes. Jack is deeply upset by the prison term so much so that he turns violent, where he starts fighting the wardens and his fellow inmates. He fakes insanity, gets admitted to a mental institution, due to his state of madness, and, thereafter, he escapes from the Mathare Mental Hospital. His freedom, however, lasts for only a few hours before he is apprehended and taken back to prison. This does not break Jack Zollo as he still remains strong in his spirit and tries to survive the harsh conditions in jail, where he eats only one potato each day. In prison, Zollo tells of his adventures, how he was constantly at war with the agents of the state and how he conquered the city.
In the city, he has to constantly flee from the agents of law and order in order for him to avoid prison. Zollo seems to celebrate a life that is well led and one that he is determined to continue living with in prison against all odds. In fact, Zollo gains popularity in prison both with his fellow inmates and the prison authorities, and he equally maintains his heroic position throughout his life in prison. Zollo comes out as a person who has had his privileges in prison, and in the city, owing to his reputation as a successful criminal. Prison becomes Zollo's city and to him, there is no boundary between prison and the city.
---------------------------
Learn Swahili with SwahiliPod101!
Don't forget to stop by SwahiliPod101.com for more great Swahili Language Learning Resources!