Share Pangani FM Podcasts
Share to email
Share to Facebook
Share to X
Karibu kusikiliza Makala ya Nitunze Nikutunze.
Makala hii huruka kila siku ya Ijumaa kuanzia saa 1 na Nusu Usiku kupitia Pangani FM ikiwa kwa lengo la kujadili Athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi na kutafuta njia mbadala ya kukabiliana nayo pamoja na njia salama ya kuhifadhi taka na kutunza mazingira kwa Maendeleo Endelevu.
Episode hii ya Nitunze Nikutunze inaangazia juu ya swala Zima la kulinda Tabaka la Ozoni kwa ustawi wa mazingira na Viumbe Hai.
Katika jitihada za kuhifadhi tabaka la ozoni mwaka 1996 Serikali ya Tanzania iliandaa na kutekeleza Programu ya Taifa ya kuondosha matumizi ya kemikali zinazomong'onyoa tabaka la ozoni nchini.
Kama sehemu ya jumuiya ya kimataifa hadi sasa Tanzania imeweza kupunguza zaidi ya tani 216 sawa na asilimia 86 ya kiasi cha matumizi ya kemikali zinazomong'onyoa tabaka la ozoni.
katika jitihada za kuhifadhi Tabaka la Ozoni, mwaka 1996, Serikali ya Tanzania iliandaa na kutekeleza Programu ya Taifa ya kuondosha matumizi ya kemikali zinazomong’onyoa tabaka la ozoni ili kuhakikisha kwamba hakuna sekta ya uchumi au jamii inaathirika kutokana na matakwa ya Itifaki ya Montreal. Aidha, programu hii ilianzisha utaratibu wa kusimamia na kudhibiti uingizaji wa kemikali na bidhaa zenye kemikali zinazoharibu tabaka la Ozoni kutoka nje ya nchi.
kipindi hiki kimejadili maana ya Tabaka Ozoni, athari zake na namna ambavyo linamhusu kila mtu katika maisha yake ya kila siku na jukumu la Jamii katika kutunza Tabaka Ozoni.
Ndani ya Kipindi hiki utamsikia Afisa mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Muuungano na Mazingira nchini Tanzania Pamoja na sehemu ya Hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. George Simbachawene katika Maadhimisho ya katika Siku ya Kimataifa ya Hifadhi ya Tabaka la Ozoni,Maadhimisho yaliyofanyika Jijini Dodoma siku ya Tarehe 17 mwezi Septemba mwaka 2020.
Leo Oktoba 16-2020 Tanzania ikiungana na Mataifa mengine ulimwenguni kuadhimisha Siku ya Chakula Duniani.
kauli mbiu ya Mwaka huu inasema “Kesho Njema Inajengwa na Lishe Bora Endelevu”
karibu kusikiliza mahojiano maalum aliyofanya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba kupitia kipindi cha Asubuhi ya leo kinachoruka Pangani FM
Leo October 14 mwaka 2020 ni Kumbukizi ya Kitaifa ya miaka 21 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kilichotokea Oktoba 14, 1999 nchini Uingereza alipokuwa anapatiwa matibabu.
Mwanahabari wetu Rajabu Mustapha Mrope ameandaa Makala Fupi iliyobeba Historia ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Leo October 14 mwaka 2020 ni Kumbukizi ya Kitaifa ya miaka 21 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kilichotokea Oktoba 14, 1999 nchini Uingereza alipokuwa anapatiwa matibabu
Mwalimu Nyerere ni mmoja kati ya waasisi wa Taifa la Tanzania, ambaye alishiriki kikamilifu katika harakati za kulikomboa Taifa kutoka kwa ukoloni wa Waingereza
Alikuwa Rais wa kwanza wa Tanganyika na aliongoza tangu Taifa lilipopata Uhuru, Desemba 9, 1961 hadi mwaka 1985
Alikuwa na Falsafa ya Ujamaa na kujitegemea ambapo aliamini ili Taifa liendelee kunahitajika watu, ardhi, Siasa safi na Uongozi bora.
Katika kuadhimisha siku hii kwa kina mwandishi wetu Erick Mallya amefanya mahojiano na Madaraka Nyerere ambaye ni mtoto wa Hayati Mwalimu julius kambarage Nyerere..
karibu katika 'Kona ya Kijanja'
Ni muendelezo wa kona ya kijana kipindi chenye lengo la kuwawezesha vijana kujenga uelewa na kuchukua hatua dhidi ya ukatili,usawa wa kijinsia pamoja na maendeleo yao.
Kipindi hiki hukujia kila siku ya alhamisi kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa mbili kamili jioni na kurudiwa siku ya jumamosi kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 12:30 jioni.
Episode hii ya Kona ya Kijanja inayamulika maisha ya vijana wanaofanya Shughuli ya 'bodaboda' na namna wanavyoitumia katika kujikwamua kiuchumi.
Usafi wa mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu kuanzia katika ngazi ya Familia, Jamii, Asasi mbalimbali za kitaifa na Kimataifa pamoja na serikali.
Hii ni kutokana na kwamba usalama wetu katika Mazingira huchangia ulinzi dhidi ya maradhi, majanga na athari nyingine zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi bila kusahau ukweli kwamba Utunzanji wa mazingira huchochea maendeleo endelevu.
Episode hii ya Nitunze Nikutunze inaangazia juu ya jitihada za wananchi katika utunzaji wa mazingira yanayo wazunguka huku ikiakisi athari za kutotunza mazingira hayo.
Nyumba ni choo! Huu ni usemi ambao hutumika mara nyingi ukiangazia umuhimu wa choo bora na huduma za kujisafi nyumbani.
Hii ni Makala ya nitunze nikutunze …popote ulipo tunakualika kusikiliza Makala hii kila siku ya ijumaa kuanzia saa 1:30 hadi saa 2:00 usiku.
Lengo ikiwa ni kujadili athari za mabadiliko ya tabia nchi na kutafuta njia mbadala ya kukabiliana nayo pamoja na njia salama ya kuhifadhi taka na kutunza mazingira kwa maendeleo endelevu.
Episode hii ya Makala ya nitunze nikutunze inaangazia swala zima la kukosekana kwa Vyoo kunavyochangia uharibifu wa Mazingira. mazingira
Tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, 1992 nchi yetu imekuwa ikifanya uchaguzi wa viongozi mbalimbali wakiwemo Rais, Wabunge na Madiwani kila baada ya miaka mitano au kwa mujibu wa sheria pale itakapo hitajika.
Wananchi hupata nafasi ya kuelimishwa umuhimu wa kushiriki uchaguzi kwa kupiga kura au kuwa wagombea wa nafasi mbalimbali. Haki ya kuchagua na kuchaguliwa ni haki ya msingi inayotolewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mahojiano haya kati ya Mwanahabari Wetu Erick Mallya na Jenerali Ulimwengu yamelenga kuhoji Je wananchi wanafuatilia au kuhoji juu ya utekelezaji wa ahadi wanazopewa na wagombea wakati wa kampeni za uchaguzi?
Eid el Fitr mwaka huu Pangani FM iliwakutanisha Wasanii mbalimbali akiwemo kassim Mganga
amezungumzia mengi ikiwemo Manuari Band, kusimama kutoa kazi mpya, kucheza karate, na mengine mengi
Enjoy
Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2020 Pangani FM inaangazia juu ya namna ambayo wananchi wanaweza kumpata kiongozi wanayemhitaji.
kipindi kimewakutanisha wanachi pamoja na Makatibu wa Vyama vya Siasa Wilayani Pangani.
The podcast currently has 12 episodes available.