Kwa Mujibu wa Ripoti mpya za shirika la Afya Duniani (WHO) zinasema kuwa ugonjwa wa shinikizo la damu ndio ugonjwa ambao unaathiri watu wengi zaidi barani Afrika huku ikionesha asilimia zaidi ya 10 ya Waafrika wameshapata na ugonjwa huo.
Huku sababu kubwa zikitajwa kutokana na watu wengi hivi karibuni kupuuza kufanya mazoezi, kupunguza au kutotumia kabisa matunda angalau matano na mboga kwa siku, matumizi ya tumbaku au sigara na pombe
Kipindi cha Siha Njema kwa juma hili kinangazia juu ya hali ya ukubwa wa tatizo hili katika jamii zetu lakini pia sababu ambazo zimechanga katika ongezeko kwa tatizo hili