Neno U.T.I ambalo ni ni kifupisho cha Urinary Tract infections,ambayo kwa lugha yetu ni maambukizi ya njia ya mkojo si geni katika masikioni mwa wengi,
Ni tatizo kubwa ambalo hivi karibuni limetajwa kusumbua zaidi watoto wa kike na wanawake haswa kwa wanafunzi wanaotumia vyoo vya jumuiya.
Basi leo kwa mara nyingine kupitia Makala yetu ya Siha Njema tutazungumzia juu ya tatizo la maambukizi katika njia ya mkojo Urinary Tract Infection,tatizo ambalo hivi karibuni linawasumbua sana watoto na wanawake