Mara nyingi watu wawili wanapochumbiana, huwa kuna msukumo wa kuichokora simu ya mwenzako mfano kuangalia jumbe, kuona picha alizo nazo katika simu, mawasiliano anayofanya na kadhalika. Lakini je, ni sawa kuwa na uhuru wa kuichokora simu ya mpenzi wako ama huenda hali hiyo ikazua mgogoro? Beatrice Maganga amelizamia suala hili akizihusisha kauli za wananchi vilevile hoja za Mwanasosholojia, Alex Munyere.