Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, CSW69 unafikia tamati hii leo Machi 21 hapa katika makao makuu, na wakulima wanawake nchini Senegal. Mashinani inatupeleka nchini Tanzania kumulika mradi wa maji.Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, CSW69 unafikia tamati hii leo Machi 21 hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Bi. Gertrude Mongella, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa wanawake maarufu kama Mkutano wa Beijing uliofanyika mnamo mwaka 1995, hivi tunavyozungumza, pamoja na umri wake mkubwa ameshirikia karibia vikao vyote vya mkutano huu wa CSW69 ambao pia ulikuwa unaangazia utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa miaka 30 iliyopita chini yake mama Mongella.Tukiwa bado ndani ya mwezi wa Machi, unaotambuliwa kuwa ni mwezi wa wanawake tunakwenda nchini Senegal ambako huko wasichana waliokuwa wakifanya kazi za ndani, wamewezeshwa na Umoja wa Mataifa na sasa ni wakulima na wanatumia stadi za upigaji na utengenezaji video za mtandaoni kuelimisha jamii kuhusu kilimo chenye tijaMakala inayoturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwenye mkutano wa Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani CSW69 unaokunja jamvi hii leo Flora Nducha amebahatika kuzungumza na mmoja wa washiriki wa mkutano huo kutoka asasi za kiraia nchini Tanzania.Na katika mashinani fursa ni yake Janeth Zakaria kutoka kijiji cha Kaguruka mkoani Kigoma nchini Tanzania ambaye kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF anasema alikuwa anatembea umbali wa kilomita 10 kupata maji safi na salama lakini sasa ni hatua chache tu kutoka nyumbani kwake”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!