"Nikamuuliza, Ngila utaniua na unimalize? Akaniambia umeongea kwa mara ya kwanza na ya mwisho, akaendelea na kunikatakata.'' Jackline Mwende mwenye umri wa miaka 32 anaanza kusimulia mahangaiko yanayomkumba baada ya mumewe kumkata mikono yote miwili.
Ilikuwa Jumamosi Julai 23, mwaka 2016 Mwende aliporejea nyumbani usiku alikokuwa akiishi peke yake kwa sababu mumewe alikuwa ametoweka kwa miezi mitatu.
Kwa miaka mingi, Mwende na mumewe Stephen Ngila waliishi bila kujaaliwa mtoto hali iliyosababisha matatizo katika ndoa yao. Ilisemekana Ngila alimshambulia Mwende kwa kumkatakata kwa upanga alipobaini kwamba alikuwa na mpenzi mwingine.
Fahamu zaidi katika podcast hii kuhusu kilichotokea usiku huo, alivyookolewa na aliko Stephen Ngila.