Dickson Kibiwott alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Masinde Muliro takriban miaka 5 iliyopita alipougua ghafla.
Alipatakina na tatizo la kiafya ambapo kinga ya mwili hushambulia seli mwilini, ugonjwa ambao unajulikana kama multiple sclerosis, ambao ulimlemaza baada ya siku tatu tu.
Ugonjwa huu hauna tiba na wakati mwingine humsababisha mtu kupooza, kukosa kuona vizuri, kuhisi uchovu mwingi, kushindwa kutafuna chakula na kumeza, kushindwa kuzungumza miongoni mwa matatizo mengine mengi.
Kibiwott alilazimika kusitisha masomo yake na mamaye akilazimika kusitisha biashara ili kumshughulikia akiwa nyumbani.
Faith Kutere amezungumza na Kibiwott pamoja na mamaye, Loice Tum anayeeleza changamoto za kumshughulikia mwanawe ambaye ni mtu mzima kama mtoto mdogo baada ya ugonjwa huo kumlemaza.