Je, unajua nini kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu yaani TB? Umewahi kusikia kwamba TB pia huathiri mifupa? Doris Sambu, mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Multimedia ana ulemavu wa mguu kutokana na TB ya mifupa. Doris, anasema alianza kuugua akiwa na umri wa miaka 7.
Anasema mamaye alipompeleka katika Hospitali ya Londiani, Kericho, ugonjwa huo haukutambuliwa hali iliyomlazimu kukaa hospitalini kwa muda hadi pale alipopelekwa katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta KNH, jijini Nairobi. Alipokuwa KNH ndipo ilipobainika kwamba alikuwa akiugua TB ya mifupa kisha akafanyiwa upasuaji katika paja. Licha ya juhudi za madaktari, mguu wake ulilemaa.
Anasema mbali na ulemavu huo kumsababishia changamoto nyingi kama vile msongo wa mawazo, uhusiano wake wa kimapenzi umesambaratika kutokana na hali hiyo. Hata hivyo, amepiga moyo konde na kuendelea na maisha kama kawaida.‚Äč Amezungumza na Esther Kirong katika makala haya.