Hujambo msikilizaji wa Nukta the Podcast, karibu katika mfululizo wa episode zetu maalumu zinazoangazia Usimamizi wa rasilimali maji pamoja na mazingira katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania.
Katika sehemu hii tutamulika hatari inayoukabili Mto Ngerengere uliopo mkoani Morogoro kutokana na uchafuzi unaofanywa wa mto huo.
Pia tutachambua hatua zilizochukuliwa na zinazotakiwa kuchukuliwa ili kuunusuru mto huo unaopita Morogoro mjini.
Mimi ni Esau Ezra Ng’umbi kwa niaba ya mtayarishaji wa makala hii Daniel Samson, pamoja na mhariri wetu, Nuzulack Dausen, ninakukaribisha kuungana nami mpaka tamati.