Mtu anayemwamini Yesu Kristo, na mafundisho yake, hana haja ya kuogopa kifo. Yesu alikuja kutuweka huru, kwa hiyo sisi tunaoamini siyo watumwa tena. Waebrania 2:14,15 imesema “Basi kwa kuwa watoto wana nyama na damu, Yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kifo chake, apate kumwangamiza huyo mwenye nguvu za mauti, yaani, Shetani, na kuwaweka huru wale waliokuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa mauti.”
Kwa hiyo, tunajua kwamba kuwa huru katika Kristo Yesu inamaanisha pia tusiogope kifo. Sikiliza kipindi hiki uelewe zaidi tukianzia na maneno ya Yesu kwamba “Amin, amin, nawambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele” (Yohana 6:47). Uzima wa milele maana yake hakuna kifo.